TIA MARATHON YAIFIKIA YAS

October 17, 2025
    Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) imefanya ziara katika makao makuu ya YAS yaliyopo katika jengo la PSSF Tower jijini Dar es Salaam, ikiwa na lengo la kujenga na kuimarisha ushirikiano kuelekea maandalizi ya msimu wa pili wa TIA Marathon 2025.

Ugeni huo uliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa TIA, Prof. William Pallangyo, ambaye alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya taasisi hizo katika kusaidia wanafunzi wa TIA pamoja na jamii kwa ujumla. Prof. Pallangyo alibainisha kuwa ushirikiano huo utaendelea kuchochea mafanikio kupitia kauli mbiu ya mbio hizo: “Run, Inspire and Support.”

Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa YAS, Bw. Norman Kiondo, aliupokea ugeni wa TIA na kushiriki mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano na kuboresha maandalizi ya TIA Marathon 2025. Mazungumzo hayo yalijikita katika kubainisha mbinu bora za kuendeleza ushirikiano baina ya taasisi hizo kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla.

TIA Marathon 2025, msimu wa pili, imepangwa kufanyika jijini Dar es Salaam, ikiwa na dhamira ya kuhamasisha, kuunga mkono na kuleta mabadiliko chanya katika jamii. Kupitia tukio hili, TIA na YAS zinalenga kuendelea kuchangia katika ustawi wa jamii na kutoa huduma bora zaidi kwa taifa na wadau wao.

 
Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

Tanga campus

Zanzibar Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/