KIKAO CHA MARIDHIANO KUKAMILIKA KWA UJENZI WA JENGO LA TAALUMA LA TIA SINGIDA IFIKAPO JUNI 2026

October 14, 2025
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo, leo ameiongoza kikao cha kazi kilichowahusisha maafisa wa TIA, mkandarasi mshauri OGM Consultants, mkandarasi wa ujenzi Salem Construction Limited, pamoja na wataalamu wa masuala ya mazingira na kijamii.

Kikao hicho kilijadili mikakati na makubaliano na mkandarasi Salem Construction Limited ili kuhakikisha kuwa mradi wa ujenzi wa Jengo la Taaluma unakamilika ifikapo Juni 2026.

Mradi huu, wenye thamani ya shilingi bilioni 13.5, unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa HEET chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia. Ujenzi wa jengo la ghorofa tatu unajumuisha madarasa ya kisasa, ofisi, na kumbi za mihadhara, likiwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi zaidi ya 3,600 kwa wakati mmoja.

Prof. Pallangyo alisema: “Mradi huu ni zaidi ya jengo; ni uwekezaji wa kimkakati katika mustakabali wa elimu ya juu nchini Tanzania. Tunatarajia kuwa miundombinu hii itaimarisha uwezo wetu wa kutoa elimu bora na shindani kimataifa.”

Ujenzi huu unatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, na kuimarisha ubora wa elimu ya juu nchini.

Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

Tanga campus

Zanzibar Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/