TAASISI YA UHASIBU TANZANIA (TIA) YASAINI MAKUBALIANO YA MASHIRIKIANO NA KAMPUNI ZA JM INVESTMENT, TUKIIO NA BASIL LINK COMPANY LTD

September 6, 2025

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William A. Pallangyo, amesaini mikataba ya makubaliano ya mashirikiano na kampuni tatu: JM Investment, Tukiio, na Basil Link Company Ltd, kwa ajili ya maandalizi ya TIA Marathon msimu wa pili leo tarehe 04 Septemba, 2025

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini, Prof. Pallangyo amesema kuwa lengo kuu la TIA marathoni ni kukuza afya, kuimarisha mshikamano, na kuhamasisha uwekezaji katika elimu bora kwa vijana wa Kitanzania.

“Lengo letu ni kuchangisha fedha kwa ajili ya kuwasaidia wanafunzi wasiojiweza, wakiwemo mabinti waliopata ujauzito wakiwa katika umri mdogo, watu wenye ulemavu kwa kuwapatia vifaa kama viti mwendo, pamoja na wale wenye uoni na usikivu hafifu,”alisema Prof. Pallangyo.

Aidha, alieleza kuwa marathoni hiyo ni fursa ya jamii kuungana, kuhamasika, na kuonyesha kuwa elimu na afya ni mambo yanayokwenda pamoja.

 

 

Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

Tanga campus

Zanzibar Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/