TUENDELEE KUITANGAZA TIA INAYOTOA ELIMU KWA UFANISI” Profesa Pallangyo

June 10, 2022
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Profesa William A. Pallangyo leo ametembelea  maonesho ya Mafunzo ya Vyuo vya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TVET) yanayoendelea katika Viwanja vya Jamhuri, Dodoma.
Profesa Pallangyo amesema TIA tuendelee kutangaza majukumu makuu ya Taasisi kwa Umma, kwenye nyanja bobezi za Mafunzo,Tafuti na Ushauri ili kuwa na Wanafunzi bora watakaopata elimu yenye Ufanisi itakayowaandaa kujiajiri na kuajiriwa
“Leo kwenye maonesho haya mefurahi kumuona Kijana wa TIA kutoka Kampasi ya Mbeya Gift Lutumo ambaye ni Mkulima, tena katika umri mdogo na anatoa elimu ya Parachichi kwenye banda letu ambayo ina Soko kubwa Marekani, hili ni la kujivunia sana,”. Alisema Profesa Pallangyo
Taasisi ya Uhasibu Tanzania inakukaribisha katika Banda lake Viwanja vya Jamhuri  geti la Nyuma upande wa kushoto kwenye kona ya Goli la mwisho.
Katika Banda hili utapata huduma za Udahili kama Kozi zinazotolewa,ushauri wa kozi za kusoma kulingana na ufaulu wa Mwanafunzi kuanzia ngazi ya cheti cha awali, Stashahada, Shahada ya Kwanza, Stashahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamili, pia utapata huduma za Utafiti na Ushauri wa kitaalam.
Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
MAB Members
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/