TIA NA MAENDELEO YA MIUNDOMBINU 

July 25, 2022
Afisa Mtendaji Mkuu Taasisi ya Uhasibu Tanzania Prof. William A. Pallangyo akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mipango Wizara ya Fedha na Mipango Ndugu Moses Dulle wametembelea mradi wa ujenzi Kampasi  ya Mwanza katika eneo la Nyang’homango Misungwi jijini Mwanza.
Mradi huo unaohusisha ujenzi wa Jengo la Taaluma lenye madarasa 9 yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1100, jengo la utawala lenye ofisi 16, Maabara ya kisasa ya Kompyuta yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi 200 pamoja na Maktaba kubwa ya kutumiwa na wanafunzi 250 kwa wakati mmoja,  kukamilika kwa majengo hayo kutaongeza udahili na kurahisisha mazingira wezeshi ya kusomea na kufundishia.
Ujenzi wa mradi huu unathamani ya shilingi za kitanzania bil 7.8 fedha  ambazo  TIA imefadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Wizara ya Fedha na Mipango.
Katika ziara hiyo pia waliambatana na Makamu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala TIA – Dkt. Issaya Hassanali, pamoja na Maafisa waandamizi kutoka TIA na Wizara ya Fedha na Mipango.
                                         
                                        
                                         
Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
MAB Members
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/