TIA KAMPASI YA KIGOMA YAKABIDHIWA GARI

July 26, 2022

Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Prof. William A.Pallangyo amemkabidhi gari  Kaimu Meneja wa Kampasi ya Kigoma Mhadhiri Martin Mnyili, leo katika Kampasi ya Singida.

Wakati akimkabidhi gari hilo, Prof.Pallangyo amesisitiza utunzaji wa magari hayo kwani yananunuliwa ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu mbalimbali ya Taasisi.

Naye, Mhadhiri Martin Mnyili ameishukuru Taasisi kwa kumpatia kitendea kazi muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya kampasi ya Kigoma na kuahidi kuitunza vyema.

Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na baadhi ya viongozi ambao wapo SINGIDA kwa kazi maalum za Taasisi pamoja na Wafanyakazi wengine wa TIA.

Taasisi ya Uhasibu Tanzania inaendelea kuboresha mazingira rafiki ya utoaji huduma ya kufundishia na kusomea Ili kuendelea kutoa elimu yenye ufanisi.

 

Vision and Mission
Core Values
Main Functions
Why Choose TIA
MAB Members
Online Application
Online Registration
LMS

Dar campus

Mbeya Campus

Singida Campus

Mtwara Campus

Kigoma Campus

Mwanza Campus

 

History

Services

TIA Journal

TIA Repository

Open Access DB

Subscribed DB

Catalog

 

/*** Collapse the mobile menu - WPress Doctor ****/