Afisa Mtendaji Mkuu Prof.William Pallangyo akiambatana na Makamu Mkuu wa Chuo Fedha,Utawala na Mipango Dkt.Issaya Hassanal, Meneja Miliki Mhandisi Masuhuko Nkuba na Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi Geofrey Magembe pamoja na mwenyeji wao Dkt. Godwin Mollel Kampasi Meneja leo  wametembelea ujenzi wa mradi wa majengo 5 unaoendelea Kampasi ya Mtwara.
Ukamilishaji wa mradi huu utaenda kuboresha miundombinu ya kusomea na kufundishia kwa zaidi ya Wanachuo 600 Kampasi ya Mtwara kwa mwaka wa Masomo 2023/2024.







